Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Operesheni za amani mipakani Ethiopia/Eritrea zatathminiwa upya na BU

Operesheni za amani mipakani Ethiopia/Eritrea zatathminiwa upya na BU

Wajumbe wa Baraza la Usalama walikutana kwenye kikao cha faragha, mapema wiki hii, kwa muda wa saa tatu, kushauriana juu ya marekibisho yanayotakikana kuchukuliwa na jumuiya ya kimataifa kuhusu shughuli za vikosi vya UNMEE vinvyohudumia ulinzi wa amani mipakani Ethiopia na Eritrea. Wajumbe wa kimataifa katika Baraza la Usalama wamependekeza kuitishwe kikao chengine wiki ijayo kufuatilia mazungumzo magumu ya kuamua kama UM uendelee kusimamia utekelezaji wa maazimio ya kusitisha mapigano mipakani kati ya Ethiopia na Eritrea au la.