Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Shambulio dhidi ya kiongozi wa Afghanistan lashtumiwa na KM

Shambulio dhidi ya kiongozi wa Afghanistan lashtumiwa na KM

KM Ban Ki-moon ameshtumu vikali shambulio liliotukia Ijumapili katika mji wa Kabul, Afghanistan, dhidi ya Raisi Hamid Karzai wakati alipokuwa akiangalia paredi ya ushindi. Shambulio hilo pia lilisababisha vifo vya wanabunge wawili, na kuwajeruhi wanabunge tisa wengine, kitendo ambacho KM alisema kinaharamisha kabisa maadili ya kiutu.