Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM anasailia mgogoro wa chakula na viongozi wa mashirika ya UM

KM anasailia mgogoro wa chakula na viongozi wa mashirika ya UM

KM Ban Ki-moon ameanza mazungumzo maalumu katika mji wa Bern, Uswiss na wakuu wa mashirika 27 ya kimataifa yenye kuhudumia shughuli za maendeleo. Lengo la mjadiliano hayo ni kusailia kipamoja hatua za kuchukuliwa kukabiliana na mgogoro hatari uliotokana na kupanda kwa kasi kwa bei za chakula, na nishati, katika soko la kimataifa katika wiki za karibuni.