Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Dola milioni 500 zahitajiwa na WFP kufidia mfumko wa bei ya chakula ulimwenguni

Dola milioni 500 zahitajiwa na WFP kufidia mfumko wa bei ya chakula ulimwenguni

Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetuma kwa Serikali Wanachama barua ya “ombi la dharua, na lisio la kawaida” linalopendekeza lifadhiliwe haraka dola milioni 500 mnamo wiki nne zijazo, ili kuepukana na hatari ya ulazima wa kupunguza huduma za ugawaji vyakula “kwa ule umma unaotegemea misaada hiyo kunusuru maisha”. Taarifa ya WFP imedhihirisha kukabiliwa na upungufu mkubwa wa fedha na haimudu tena kununua chakula kwa sababu ya kuzuka, hivi karibuni, mfumko mkubwa wa bei za chakula katika soko za kimataifa.