Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF imelaani utekaji nyara wa wahandisi Darfur Kaskazini

UNICEF imelaani utekaji nyara wa wahandisi Darfur Kaskazini

Shirika la Umoja wa Mataifa juu ya Mfuko wa Maendeleo ya Watoto (UNICEF) limelaani kitendo haramu cha utekaji nyara katika eneo la Um Tajok, Darfur Kaskazini, na kutorosha kundi la wahandisi wanne wanaotumikia Shirika la Maji la Taifa Sudan pamoja na madereva wao wanne, na pia magari na vifaa vya kuchimbia maji.