UM imeidhinisha mapatano ya msingi na Serikali ya Chad kuhusu ulinzi wa amani nchini
Mnamo mwisho wa wiki iliopita Shirika la Ulinzi wa Amani la Umoja wa Mataifa katika Chad na Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINURCAT) limetia sahihi na wenye madaraka, kwenye mji mkuu wa N’Djamena, Chad, maafikiano ya msingi wa kanuni za kuendesha operesheni zake katika Chad.