Mtuhumiwa wa jinai ya halaiki Rwanda ajisalimisha kwa ICTR
Leonodis Nshogoza ameripotiwa kujisalimisha, kwa khiyari, mbele ya Mahakama ya Kimataifa juu ya Rwanda (ICTR) iliopo mjini Arusha, Tanzania baada ya kutolewa ilani ya kimataifa ya kumshika. Nshogoza alishtakiwa kushiriki kwenye jinai ya vita Rwanda katika miaka ya tisini. Hivi sasa Nshogoza yupo kizuizini chini ya hifadhi ya Mahakama ya ICTR akisubiri kesi.