Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kiongozi wa waasi Kongo amekamatwa na kupelekwa Mahakama ya ICC Hague

Kiongozi wa waasi Kongo amekamatwa na kupelekwa Mahakama ya ICC Hague

Mathieu Ngudjolo Chui, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) anayedaiwa kuongoza kundi la waasi la National Integrationist Front (FNI) amekamatwa kati ya wiki na kuhamishwa kwenye Mahakama ya Mauaji ya Jinai ya ICC iliopo mjini Hague, Uholanzi. Kwa mujibu wa taarifa ya Bruno Cathala, Msajili wa Mahakama, mnamo Februari 2003 mtuhumiwa Chui anadaiwa aliandaa, na kuongoza mashambulio katili kwenye kijiji cha Bogoro, kilichopo kaskazini-mashariki ya Ituri katika JKK na kusababisha vifo kadha wa kadha kwa watu wasio hatia.