Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Eritrea imezuia Walinzi wa usalama wa UM kuingia Ethiopia

Eritrea imezuia Walinzi wa usalama wa UM kuingia Ethiopia

Wenye madaraka Eritrea wamekataa kuwaruhusu watumishi wa Shirika la UM la Ulinzi wa Amani Mipakani Ethiopia/Eritrea (UNMEE) kwenda Ethiopia, hali ambayo iliwalazimisha kurejea mjini Asmara kusubiri ushauri kutoka UM juu ya hatua za kuchukuliwa nawo baada ya mvutano huu. Tukio la kuwazuia walinzi wa amani kutovuka mpaka limejiri licha ya kuwa Ijumaa iliopita Baraza la Usalama lilishtumu vikali "ukosefu wa ushirikiano" kutoka Serikali ya Eritrea, ambaye ililaumiwa kujitenga na majukumu yake ya kusaidia vikosi vya UNMEE kudhibiti bora usalama kwenye eneo la mgogoro mipakani.