Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Twachoka kusubiri', unyanyasaji wa wanawake ukomeshwe halan - KM Ban

'Twachoka kusubiri', unyanyasaji wa wanawake ukomeshwe halan - KM Ban

KM Ban Ki-moon Ijumatatu alikuwa miongoni mwa watu mashuhuri kadha walioshiriki kwenye taadhima za ufunguzi rasmi wa kikao cha mwaka cha 52 cha Kamisheni ya UM juu ya Haki za Wanawake (CSW). Kwenye risala ya ufunguzi, mbele ya wawakilishi wa kimataifa, KM Ban alichukua fursa ya kuanzisha kampeni ya kimataifa itakayojumuisha UM na mashirika yake yaliozagaa kote duniani, na kuchangisha serikali za Nchi Wanachama na jumuiya za kiraia, halkadhalika, kufyeka kidharura, na kwa nguvu moja, vitendo vyote vya unyanyasaji, utumiaji mabavu na udhalilishaji wa wanawake. Alisema vitendo karaha kama hivi dhidi ya wanawake havistahamiliki kamwe. ~~Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaa ya mtandao.