Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Polisi wa UNAMID kutoka Banglandesh waanzisha doria ya masafa marefu Darfur

Polisi wa UNAMID kutoka Banglandesh waanzisha doria ya masafa marefu Darfur

Askari wa Polisi kutoka Bangladesh wanaowakilisha Vikosi Mseto vya UM/UA kwa Darfur (UNAMID) vimeanzisha doria ya majaribio, za masafa marefu ya kilomita 200, zilizoanzia kwenye kambi zao katika mji wa Nyala, Darfur Kusini na kuendelea hadi mji mkuu wa Darfur Kaskazini wa El-Fasher.