Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utekelezaji wa MDGs Kijijini Mbola, Tanzania - Kilimo na Mazingira (Sehemu ya Pili)

Utekelezaji wa MDGs Kijijini Mbola, Tanzania - Kilimo na Mazingira (Sehemu ya Pili)

Wasikilizaji, kwenye makala ya kwanza kuhusu huduma za wanavijiji wa Mbola, katika Mkoa wa Tabora, Tanzania za kuyakamilisha yale Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) kwa wakati, tulikupatieni dokezo na fafanuzi za Kaimu Naibu wa Kilimo na Mazingira, Eliezer N. Kagya ambaye anasimamia utekelezaji wa malengo hayo kwenye eneo husika. Alielezea namna wanavijiji wanavyoshiriki na kushirikishwa kwenye huduma za pamoja za kuondosha njaa kwenye eneo lao, kwa kutumia kilimo cha kisasa. Kwenye sehemu ya pili ya mazungumzo yetu, Kagya anazingatia matokeo ya aina gani yatakayojiri katika mwaka wa pili, kwenye sekta ya kilimo na mazingira, baada ya kuanzishwa mradi huu muhimu wa MDGs wenye lengo la kuondosha njaa na kuimarisha maendeleo ya kuchumi na jamii yatakayokuwana natija kwa wote.