ICTR yafungua mashtaka, kwa mara ya awali, kwa ushahidi wa uongo
Mahakama ya ICTR, kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa, imefungua mashtaka kwa shahidi fulani aliyetoa ushahidi wa uwongo kwenye kesi ya aliyekuwa Waziri wa Ilimu wa Rwanda, Jean de Dieu Kamuhanda, ambaye alishtakiwa kushiriki kwenye mauaji ya halaiki yaliotukia nchini mwao katika 1994. Jina la mshtakiwa wa ushahidi wa uongo bado halijadhihirishwa rasmi hadharani.