Baraza la Usalama kuzingatia, kwa mara ya kwanza, athari za mabadiliko ya hali ya hewa duniani
Wataalamu wa kimataifa katika fani ya sayansi wanaashiria ya kuwa mali ya asili ya maji, pamoja na ardhi, zitaendelea kuadimika polepole katika siku zijazo. Kadhalika inakhofiwa mabadiliko ya hali ya hewa, hali kadhalika, kama hayajadhibitiwa mapema, huenda yakazusha maangamizi yasiorudishika na kugeuza milele sura ya sayari yetu.
Sikiliza taarifa ziada juu ya mjadala wa Baraza la Usalama kwenye idhaa ya mtandao.