FAO imeitahadharisha Nigeria kuboresha udhibiti wa mifugo na kujikinga na H5N1
Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limependekeza kwa Serekali ya Nigeria kuongeza huduma za kudhibiti afya katika masoko na mashamba ya kuku, kwa kuchanja mifugo ili kujikinga na hatari ya kutapakaa kwa virusi vya aina ya H5N1, ambavyo husababisha homa ya mafua ya ndege.