Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jean-Marie Guehenno awaarifu waandishi habari juu ya vikosi vya UM kwa Darfur.

Jean-Marie Guehenno awaarifu waandishi habari juu ya vikosi vya UM kwa Darfur.

Makamu KM juu ya Operesheni za Amani za UM, Jean-Marie Guehenno aliwaarifu waandishi habari wa kimataifa katika Makao Makuu kwamba ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kufanyisha mazungumzo ya hali ya juu na Serekali ya Sudan ili kuondosha hali ya kutofahamiana na kutoaminiana, pindi tumenuia kuwasilisha mafanikio ya kudumu kuhusu pendekezo la kutuma majeshi ya amani ya UM katika Darfur, Sudan.