14 Julai 2006
Makamu KM juu ya Operesheni za Amani za UM, Jean-Marie Guehenno aliwaarifu waandishi habari wa kimataifa katika Makao Makuu kwamba ni muhimu kwa jamii ya kimataifa kufanyisha mazungumzo ya hali ya juu na Serekali ya Sudan ili kuondosha hali ya kutofahamiana na kutoaminiana, pindi tumenuia kuwasilisha mafanikio ya kudumu kuhusu pendekezo la kutuma majeshi ya amani ya UM katika Darfur, Sudan.