Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama kuidhinisha maandalizi ya vikosi vya amani kupelekwa Chad na JAK

Baraza la Usalama kuidhinisha maandalizi ya vikosi vya amani kupelekwa Chad na JAK

Baraza la Usalama limeipa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya idhini ya kuandaa ratiba halisi itakayozingatia uwezekano wa kupeleka, shirika, askari polisi na wanajeshi katika mataifa ya Chad na Jamhuri ya Afrika ya Kati, kuwapatia hifadhi bora raia walioathirika na mzozo uliodondokea maeneo jirani na Darfur, Sudan. Baraza la Usalama limependekeza kupelekwa vikosi vya ulinzi wa amani kwa mwaka mmoja kuwapatia hifadhi ya kihali wahamiaji na watu waliohajiri makwao na raia husika waliopo Chad mashariki na kaskazini-mashariki ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (JAK), na vile vile kuhakikisha wanapatiwa misaada ya kiutu kwa wakati.