BK lazingatia hatua za kuyafikia Malengo ya Milenia (MDGs) kwa wakati
Ijumatatu Baraza Kuu la UM limeanzisha kikao maalumu, hapa Makao Makuu, cha siku mbili, cha wawakilishi wote kujadilia taratibu za kuzijumuisha serikali za kimataifa pamoja na wadau wanaohusika na huduma za maendeleo, ili kuharakisha mchango wao wa kuyafikia yale Malengo ya Milenia (MDGs), kwa wakati, katika nchi masikini, kabla ya 2015 kumalizika.