Msemaji wa KM asisitiza, tuhumu dhidi ya walinzi wa amani katika JKK zinapotosha
Naibu Msemaji wa KM, Marie Okabe, kwenye mazungumzo na waandishi habari Ijumatatu, alikanusha madai ya ripoti za Shirika la Habari la Uingereza la BBC, kwamba walinzi wa amani wa UM katika JKK wameshiriki kwenye biashara ya magendo nchini humo.