WFP yaanza kugawa misaada ya chakula katika JKK
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) leo limeanza kugawa misaada ya chakula kwa watu 135,000, ambao walihamishwa makazi kidharura, na hivi sasa wamewekwa kwenye kambi sita za muda za wahamiaji ziliopo kwenye mji wa Goma, katika JKK.