Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yaihadharisha BU juu ya matatizo ya kuhifadhi wahamiaji duniani

UNHCR yaihadharisha BU juu ya matatizo ya kuhifadhi wahamiaji duniani

Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) asubuhi ya leo amehutubia Baraza la Usalama kuhusu vizingiti vinavyokabili shirika katika kuhudumia makumi milioni ya wahamiaji waliong’olewa makwao katika sehemu mbalimbali za dunia, kutokana na hali ya mkorogano na hatari iliopamba sasa hivi kwenye mazingira ya kimaaifa.