Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Huduma za kugawa chakula Ghaza zimesimamishwa, kwa muida, na UM

Huduma za kugawa chakula Ghaza zimesimamishwa, kwa muida, na UM

KM ameshtumu mashambulio ya vikosi vya Israel dhidi ya misafara ya malori ya UM, yaliokuwa yamechukua misaada ya kiutu kwa wakazi wa eneo la Ghaza, ambapo wafanyakazi wawili wa UNRWA waliuawa, licha ya kuwa wenye madaraka wamepatiwa taarifa kamili kuhusu misafara hiyo.