Sasa UN na AU zatekeleza ushirikiano kwa vitendo
Amani na Usalama
Umoja wa Mataifa, UN na Muungano wa Afrika, AU wameamua kushirikiana kwa kina ili kusaka suluhu kwenye mizozo na hii imeanza kutekelezwa huko Sudan ambapo ujumbe wa pamoja wa viongozi wa UN na AU uko ziarani nchini humo kutathmini utendaji wa ujumbe wa pamoja wa taasisi hizo huko Darfur, UNAMID.
Assumpta Massoi wa Idhaa hii amezungumza na Selemani Semunyu, mwandishi wa habari wa UNAMID kuweza kufahamu kwa muhtasari yaliyojiri wakati wa ziara hiyo ya Jean-Pierre Lacroix ambaye ni mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za UN na Smail Chergui, Kamishna wa amani na usalama wa AU.