Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maji yanaweza kuleta amani au kuchochea migogoro

Maji yanaweza kuleta amani au kuchochea migogoro

Pakua

Ikiwa leo ni Siku ya Kimataifa ya Maji, Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM ya nchini Kenya amezungumza na baadhi ya wakazi wa Kaunti ya Kajiado nchini humo kuhusu umuhimu wa uwepo wa maeneo mengi ya kupata maji katika jamii. Dhima ya Siku ya Kimataifa ya Maji ya mwaka huu wa 2024 ni "Maji kwa ajili ya amani" ikieleza kuwa kunapokuwa na ushirikiano katika suala la maji inaleta athari chanya kukuza maelewano, kuhamasisha ustawi na kujenga uwezo wa kukabiliana na changamoto za pamoja. 

Audio Credit
Flora Nducha/Kevin Keitany
Audio Duration
3'15"
Photo Credit
Radio Domus: Kevin Keitany