Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida 29 Septemba 2021

Jarida 29 Septemba 2021

Pakua

Karibu usikilize jarida ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kuhamasisha kuhusu upotevu na utupaji wa chakula na mwenyeji wako ni mimi ASSUMPTA MASSOI. 

Miongoni mwa utakayo sikia ni pamoja na programu ya UNICEF nchini Kenya yawasaidia watoto wa kike kurejea shuleni. 

Taasisi ya kusaidia wakimbizi wandani nchini Yemen yashinda Tuzo ya UNHCR ijulikanayo kama tuzo ya wakimbizi ya Nansen. 

Lokua Kanza, mwanamuziki nguli ndani  na nje ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye pia ni balozi wa kitaifa wa elimu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo, ametumia ziara yake katika shule ya msingi aliyosoma utotoni ili kuchagiza wanafunzi wa kike na wa kiume kupatia kipaumbele suala la elimu. 

karibu usikilize habari hizi na mengine mengi ikiwemo makala kutoka nchini Uganda. 

 

Audio Credit
Assumpta Massoi
Audio Duration
14'2"