Vita ya miaka 12 vimetuacha taaban tukipoteza matumaini: Raia Aleppo Syria
Leo ni miaka 12 kamili tangu machafuko yalipozuka Syria na kusababisha vita inayoendelea tangu mwaka 2011 iliyosambaratisha nchi hiyo na mamilioni ya raia wake. Maelfu wamepoteza maisha, mamilioni wamekuwa wakimbizi ndani na nje ya nchi yao na majanga mengine ya kila uchao yanazidi kuwaondelea matumaini raia wa taifa hilo la Mashariki ya Kati.