Utekelezaji wa sitisho la mapigano ukikaribia Gaza UN iko tayari kutoa misaada
Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya misaada ya kibinadamu yanayojiandaa kuingia Gaza leo yanaendelea kukusanya akiba ya misaada inayohitajika sana kwa eneo hilo lililokumbwa na vita huku kukiwa na ucheleweshaji wa utekelezaji wa kusitishwa kwa mapigano kwa muda na kuachiliwa kwa mateka wanaoshikiliwa na wanamgambo wa Hamas.