02 JUNI 2021
Pakua
Hii leo jaridani Leah Mushi anaanzia huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako waasi wa ADF wameshambulia kambi za wakimbizi wa ndani na kuua raia 55, UN umetoa taarifa ya kulaani. Atasalia huko huko Maziwa Makuu akimulika wakimbizi waliongia nchini Rwanda wakikimbia volkano ya Nyiragongo huko DRC na kisha atamulika pia suala la ndoa za utotoni. Makala tunamkaribisha John Kibego kutoka Uganda na mashinani ni ujumbe kutoka UNAIDS, karibu!
Audio Credit
Leah Mushi