Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vichocheo vya mafuriko na atahri zake vyamulikwa nchini Uganda

Vichocheo vya mafuriko na atahri zake vyamulikwa nchini Uganda

Pakua

Juu ya janga la kimataifa la COVID-19, nchi kadhaa Africa Mashariki na Pembe mwa Africa zinakumbana na janga la mafuriko ambalo tayari limewalazimisha wengi kupoteza makazi na hata maisha yao.

Majanga kama hayo huwa na uhusiano na hali ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Je, mafuriko haya kando na kuathiri binadamu moja kwa moja yana husika vyovyote na shughuli za kiuchumi za binadamu? Basi tuungane na John Kibego aliyevinjari kubaini vichochezi vya mafuriko kwa kufanya mahojiano na mwanamazingira Mosses Semahunge.

 

Audio Duration
3'25"
Photo Credit
UN Photos