Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

COVIDI-19 yazua changamoto za kupata huduma za afya Uganda

COVIDI-19 yazua changamoto za kupata huduma za afya Uganda

Pakua

Kuendelea kusambaa kwa virusi vya Corona, COVID-19 kumezifanya nchi kukaza uzi zaidi katika hatua za kukabiliana na mlipuko huo ikiwemo vikwazo vya watu kutembea na hatua za kuwataka kusalia majumbani. Vikwazo hivi pamoja na kusaidia kudhibiti mlipuko wa COVID-19 lakini pia vimezua changamoto zingine. Mathalani nchini Uganda ambako kuna marufuku ya watu kutembea wagonjwa wengi wameanza kupata changamoto ya kufikia huduma za afya kutokana na maagizo mapya yanayolenga kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo kama alivyobaini mwandishi wetu nchini humo John Kibego katika makala hii

Audio Credit
UN News/John Kibego
Audio Duration
3'37"
Photo Credit
UN News/ John Kibego