Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Biashara haramu ya tumbaku yaanza kubanwa

Biashara haramu ya tumbaku yaanza kubanwa

Pakua

Hatimaye itifaki ya kutokomeza biashara haramu ya bidhaa za Tumbaku imeanza kutiwa saini na hivyo kuonyesha utashi wa kisiasa wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa kudhibiti matumizi ya tumbaku. Hafla hiyo ilifanyika mjini Geneva Uswisi kwa mataifa 12 wanachama wa mkataba huo kutia saini na baadaye shughuli hiyo itahamishiwa New York, Marekani makao makuu ya Umoja wa Mataifa kwa nchi nyingine wanachama wa Mkataba huo kuweza kutia saini. Assumpta Massoi amefuatilia hafla hiyo na hii ni ripoti yake.

(SAUTI YA ASSUMPTA MASSOI)