Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ulevi na matumizi ya dawa za kulevya inaathiri afya, pata usaidizi uondokane nazo

Ulevi na matumizi ya dawa za kulevya inaathiri afya, pata usaidizi uondokane nazo

Pakua

Ripoti iliyotolewa jana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO imesema mamilioni ya vifo vinachangiwa na unywaji pombe na matumizi ya dawa za kulevya na imetoa wito wa haraka wa kutekeleza lengo namba 3.5 la Malengo ya Maendeleo Endelevu SDG la kupunguza matumizi ya pombe na dawa za kulevya na kuboresha upatikanaji wa matibabu bora kwa matatizo ya matumizi ya dawa. Halikadhalika leo ikiwa ni Siku ya Kimataifa ya kutokomeza matumizi mabaya ya madawa ya kulevya na ulanguzi wa madawa hizo Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Dawa na Uhalifu (UNODC) wamechapisha ripoti yao inayosisitiza haki ya afya kwa wote ikiomba Umoja wa Mataifa kuongza kasi katika mapambano dhidi ya matumizi ya dawa. Kevin Keitany wa redio Washirika wetu Domus FM anatupeleka nchini Kenya kufuatilia juhudi za mashirika ya kiraia na serikali hasa katika huduma za afya kwa waathirika wa madawa ya kulevya na pombe.

Audio Credit
Anold Kayanda/Kevin Keitany
Audio Duration
4'30"
Photo Credit
UN News