Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Yoga ni kiungo cha maisha na ubinadamu wetu: Guterres

Washiriki wakijumuika kwenye hafla katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kuadhimisha Siku ya 9 ya Kimataifa ya Yoga.
UN Photo/Mark Garten
Washiriki wakijumuika kwenye hafla katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York kuadhimisha Siku ya 9 ya Kimataifa ya Yoga.

Yoga ni kiungo cha maisha na ubinadamu wetu: Guterres

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Ikiwa leo ni siku ya Yoga duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema “Yoga ni kiungo, inaunganisha mwili na akili, ubinadamu na asili na mamilioni ya watu kote ulimwenguni, ambao kwao ni chanzo cha nguvu, maelewano, na amani.”

Kwa mujibu wa WHO Yoga ni mazoezi ya vioungo na pia njia yenye ufanisi ya kukabiliana na msongo wa mawazo
UN News/Elizabeth Scaffidi
Kwa mujibu wa WHO Yoga ni mazoezi ya vioungo na pia njia yenye ufanisi ya kukabiliana na msongo wa mawazo

Katika ujumbe wake maalum wa siku hii mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa  ameongeza kuwa “Katika ulimwengu hatari na uliogawanyika, manufaa ya mazoezi hayo ya kale ni ya thamani sana. Yoga inatoa fursa ya utulivu, inaweza kupunguza wasiwasi na kukuza ustawi wa akili.” 

Pia amesema yoga “Inatusaidia kuboresha nidhamu na subira. Inatuunganisha na sayari yetu, ambayo inahitaji sana ulinzi wetu. Na inafichua ubinadamu wetu wa kawaida ili kutusaidia kuelewa kwamba licha ya tofauti zetu, sisi ni wamoja.”

Na hivyo ametoa wito maalum “Katika siku hii ya kimataifa ya Yoga, hebu tukumbatie roho ya umoja, na tuazimie kujenga ulimwengu bora na wenye usawa kwa watu, sayari na sisi wenyewe.”

Tukio la Yoga katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa huko New York katika Siku ya Kimataifa ya Yoga.
UN News/ Sachin Gaur
Tukio la Yoga katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa huko New York katika Siku ya Kimataifa ya Yoga.

Siku ya kimataifa ya yoga huadhjimishwa kila mwaka Juni 21 katika sehemu mbalimbali duniani na mwaka huu hapa kwenye Umoja wa Mataifa kutakua na hafla maalum ya mazoezi ya Yoga itakayoendeshwa na waziri mkuu wa India Narendra Modi kuadhimisha siku hii.

Maudhui ya siku ya yoga mwaka huu ni “Yoka kwa ajili ya Vasudhaiva kutumbkam”  ikimaanisha “Yoga kwa ajili ya ustawi wa sayari moja, familia moja.”