Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Zaidi ya wahamiaji 1000 kutoka Afrika Mashariki wamekufa au kutoweka

Takriban waTU 1000 wamekufa kwenye njia wakijaribu kupita njia ya wahamiaji ya bahari ya Mediterania mnamo 2021
SOS Méditerranée/Anthony Jean
Takriban waTU 1000 wamekufa kwenye njia wakijaribu kupita njia ya wahamiaji ya bahari ya Mediterania mnamo 2021

Zaidi ya wahamiaji 1000 kutoka Afrika Mashariki wamekufa au kutoweka

Wahamiaji na Wakimbizi

Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji IOM limesema zaidi ya wahamiaji 1,000 wamefariki dunia au kutoweka tangu mwaka 2014 walipokuwa wakijaribu kuondoka Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika. 

Taarifa iliyotolewa na IOM kutoka Geneva Uswisi imesema wengi wa wahamiaji hao walikuwa wakisafiri kutoka Pembe ya Afrika hadi Rasi ya Uarabuni au kutoka Pembe ya Afrika kwenda Afrika Kusini.

Shirika hilo limeeleza kuwa wahamiaji wanakabiliwa na hatari kama vile usafiri wa hatari, kukosa hewa safi, vurugu, kuachwa na walanguzi wanaoahidi kuwasafirisha, ufikiaji mdogo wa huduma za matibabu na kuwekwa kizuizini.