Harakati zaendelea mashinani kuepusha mauaji ya kimbari
Kuelekea siku ya kimataifa ya kumbukizi ya waathirika wa mauaji ya kimbari na kuzuia uhalifu huo tarehe 9 mwezi huu wa disemba, makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kunafanyika tukio la kukumbuka watu hao na kuhakikisha utu kwa manusura wa vitendo hivyo.
Mkutano huo unahudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, wakati huu ambapo hata mashinani kuna harakati zinaendelea kuepusha mauaji hayo kwa kuzingatia kilichotokea Rwanda mwaka 1994.
Harakati hizo ni pamoja na zile zinazofanyika nchini Uganda ambako mwandishi wetu John Kibego amezungumza na Yusufu Bunya, msemaji wa chama cha BUKITAREPA kinachotumia vyombo vya sheria kusaka haki za jamii za watu asili za Bunyoro ili kuepuka mauaji ya kimbari na kueneza chuki za kikabila magharibi mwa Uganda, ambapo Bwana Bunya anasema..
[mahojiano]