Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Guterres alaani mashambulizi dhidi ya nyumba za ibada Indonesia

Katibu Mkuu wa UM Antonio Guterres
PICHA/UN/Evan Schneider(maktaba)
Katibu Mkuu wa UM Antonio Guterres

Guterres alaani mashambulizi dhidi ya nyumba za ibada Indonesia

Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia msemaji wake amelaani mashambulizi ya kigaidi dhidi ya  waumini kwenye nyumba za ibada 3 hii leo katika mji wa Surabaya Indonesia na kukatili maisha  raia wasio na hatia na kujeruhi wengi.

Kupitia msemaji wake, Bwana Guterres ametuma salamu za rambirambi kwa familia za wafiwa huku akiwatakia ahueni ya haraka majeruhi.


Halikadhalika Katibu Mkuu ameonyesha mshikamano wake kwa serikali ya Indonesia katika mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi na siasa za kichochezi za makundi ya wanamgambo.


Mkuu huyo  ameitaka serikali ya Indonesia kufanya uchunguzi wa kina na kuwafikisha wahusika katika vyombo vya sheria