Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wa Iraki jitokezeni kwa wingi kuwachagua viongozi wenu: Kubis

Wapiga kura katika kituo cha  Erbil, kwenye jimbo la Kurdistan, Iraq
Picha yz UNAMI/PIO
Wapiga kura katika kituo cha Erbil, kwenye jimbo la Kurdistan, Iraq

Wa Iraki jitokezeni kwa wingi kuwachagua viongozi wenu: Kubis

Masuala ya UM

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  nchini Iraq, Jan Kubis, yupo ziarani leo katika jimbo la Anbar, kwenye mji wa Fallujah  nchini humo kushuhudia mchakato wa uchaguzi wa viongozi katika ngazi mbalimbali.

Bwana Kubis ametoa wito kwa wananchi wote wa  Iraq kwenye mji wa Felluja ulioko  magharibi mwa Bagdad kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo, ili  waweze kuchagua viongozi watakaowaleta maendeleo katika jimbo hilo ambalo lilikombolewa na vyombo vya usalama vya Iraq kutoka  kwa wanamgambo wa Isis  mwaka 2016.


Viongozi wengine  wa Umoja wa Mataifa walioshuhudia zoezi la Uchaguzi nchini humo ni pamoja na Alice Walpole ambaye ni mwakilishi wa Katibu Mkuu nchini Iraq katika masuala ya siasa na uchaguzi, ambaye alitembelea kambi za wakimbizi wa ndani za Kirkuk zilizopo chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa ili kujionea zoezi la uchaguzi wa viongozi katika ngazi mbalimbali.
 
Umoja wa Mataifa umekuwa mstari wa mbele katika kutoa msaada wa hali na mali ili kufanikisha zoezi la uchaguzi wa viongozi katika ngazi mbalimbali kama vile wabunge na wakuu wa majimbo kwa ushirikiano na tume ya uchaguzi nchini Iraq NEC.