Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

DPRK imeshtumiwa na BU kwa kufanya majaribio ya makombora

DPRK imeshtumiwa na BU kwa kufanya majaribio ya makombora

Ijumatatu magharibi Baraza la Usalama (BU) lilitoa taarifa maalumu kwa waandishi habari wa kimataifa, ilioshtumu majaribio ya makombora yalioendelezwa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Umma wa Korea/Korea ya Kaskazini (DPRK) mnamo mwisho wa wiki iliopita, hali ambayo Baraza linaamini iliharamisha maazimio ya jamii ya kimataifa, na kuhatarisha usalama wa eneo pamoja na utulivu wa kimataifa.