Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahamiaji wa JKK wamiminikia Sudan Kusini kukwepa waasi wa LRA

Wahamiaji wa JKK wamiminikia Sudan Kusini kukwepa waasi wa LRA

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limetuma timu ya dharura ya maofisa watatu, kutoka ofisi yao ya Juba, na kuwapeleka eneo la Yambio, katika jimbo la Equatoria ya Magharibi, Sudan Kusini, ili kufanya ukaguzi kuhusu mahitaji ya maelfu ya wahamiaji wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) waliomiminikia huko kuanzia wiki mbili zilizopita.