Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM washiriki kwenye mkutano wa Afrika kupiga vita ubaguzi wa rangi

UM washiriki kwenye mkutano wa Afrika kupiga vita ubaguzi wa rangi

Kuanzia Ijumapili tarehe 24 Agosti (2008) maofisa wa UM pamoja na wawakilishi wa serikali za Afrika na wataalamu kutoka jumuiya za kiraia, hali kadhalika, walikutana kwenye mji mkuu wa Abuja, Nigeria kwenye kikao cha siku tatu, kuzingatia masuala yanayohusu ukabila, ubaguzi wa rangi, chuki za wageni na mifumo mengineyo inayofungamana na utovu wa kustahamiliana.