Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM imeanzisha uchunguzi wa udhalilishaji wa kijinsia katika JKK

UM imeanzisha uchunguzi wa udhalilishaji wa kijinsia katika JKK

Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (MONUC) limeripoti Ofisi ya Uchunguzi ya UM (OIOS) imeanzisha upelelezi maalumu wa kufuatilia madai ya kwamba wanajeshi fulani wa UM kutoka India walishiriki kwenye vitendo haramu vya kuajiri watoto wadogo wa kike na kujamiana nao kwa malipo. Msemaji wa MONUC, Kemal Saiki amenakiliwa akisema vitendo hivi vilidaiwa kutukia kwenye jimbo la vurugu la Kivu Kaskazini.