BU limepitisha azimio la kuisadia Usomali kupata amani
Baraza la Usalama (BU) limepitisha Alkhamisi, kwa kauli moja, azimio muhimu juu ya Usomali, azimio nambari 1814 (2008) ambalo lilimtaka KM Ban Ki-moon kuendelea na matayarisho ya ule mradi wa msingi, utakaotumiwa kuchangisha huduma za kihali na mali kutoka jumuiya ya kimataifa, ili kusaidia kurudisha tena usalama na amani nchini Usomali.