Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP inaomba isaidiwe dola milioni 256 ziada kuhudumia chakula walimwengu

WFP inaomba isaidiwe dola milioni 256 ziada kuhudumia chakula walimwengu

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetangaza mwito maalumu wenye kupendekeza kufadhiliwa na wahisani wa kimataifa dola milioni 265 ziada, ili kukidhi mahitaji ya ule umma muhitaji wenye kuhudumiwa chakula na UM, katika sehemu kadha wa kadha za kimataifa. WFP ilisema msaada huu ziada unahitajika kununua chakula kwenye soko la kimataifa kufuatilia mfumko wa kasi wa bei za chakula uliojiri karibuni.~~