Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM inawakumbuka watumishi waliofariki wakihudumia bodi la kimataifa

UM inawakumbuka watumishi waliofariki wakihudumia bodi la kimataifa

Tarehe ya leo Aprili 25 inaheshimiwa hapa Makao Makuu kama Siku Maalumu ya Kuwakumbuka Wafanyakazi wa UM waliopoteza maisha wakati wakitumikia taasisi hiyo ya walimwengu. Katika taadhima zilizofanyika kwenye bustani ya Makao Makuu, waandishi habari wenziwetu kutoka Redio ya UM, Geraldine Adams na Jerome Longue walisoma orodha ya majina ya wafanyakazi 294 waliofariki tangu Disemba 2005.