Mchochezi wa mauaji Rwanda kumalizia kifungo Utaliana
Georges Omar Ruggu, mwandishi habari wa redio aliopatikana na hatia ya kuchochea mauaji ya halaiki dhidi ya raia wenye jadi ya KiTutsi nchini Rwanda katika 1994, na ambaye alihukumiwa kifungo cha miaka 12 na Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) alihamishwa Alkhamisi kwa ndege ya kijeshi kutoka kizuizini Arusha, Tanzania na kupelekwa kifungoni Utaliana kumaliza adhabu yake.