Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwendesha Mashitaka wa ICC ameishtumu Sudan kukataa ushirikiano na Mahakama

Mwendesha Mashitaka wa ICC ameishtumu Sudan kukataa ushirikiano na Mahakama

Luis Moreno Ocampo, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya UM juu ya Jinai ya Halaiki (ICC) aliwaambia wajumbe wa Baraza la Usalama kwenye kikao cha hadhara kwamba kwa muda wa miezi 10 sasa Serikali ya Sudan imeshindwa kutekeleza pendekezo la Baraza la Usalama la kuwakamata raia wawili wa Sudan, Ahmad Harun na Ali Kushayb, na kuwapeleka Mahakamani Hague, Uholanzi baada ya raia hawa kutuhumiwa makosa ya jinai ya vita katika Darfur.