UNMIL kushirikiana na Serikali Liberia kuzalisha ajira
Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani Liberia (UNMIL), likishirikiana na Benki Kuu ya Dunia, UNDP, Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) na shirika la UM juu ya Haki za Wafanyakazi (ILO) linaendeleza mradi maalumu wa pamoja wa kujenga barabara zilizoharibiwa wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe, mradi utakaosaidia kuzalisha ajira kwa watu 50,000 vijijini. Mradi huu unaendelezwa shirika na Serikali ya Liberia, halkadhalika.