UM unatarajia matokeo mazuri Usomali
Eric Laroche Mshauri wa UM kuhusu Misaada ya Kiutu kwa Usomali alipokutana na waandishi habari wa kimataifa hapa Makao Makuu wiki hii aliashiria ya kwamba Usomali, kwa sasa, imebahatika kushuhudia “vuguvugu la mabadiliko” yaliyowapatia umma matumaini ya kwamba Serekali mpya itajinyakulia fursa ya utawala iliyobarikiwa karibuni na kurudisha amani na utulivu katika taifa ambalo limenyimwa uongozi wa Serekali halali tangu 1991.~~