Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tumedhamiria kuona uwakilishi wa dhati wa Afrika kwenye Baraza la Usalama- Waziri Monica Juma

Tumedhamiria kuona uwakilishi wa dhati wa Afrika kwenye Baraza la Usalama- Waziri Monica Juma

Pakua

Kenya ina uzoefu katika masuala ya Usalama na hiyo ni moja ya sababu ambayo imesukuma nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwania nafasi ya mwanachama asiye wa kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Hiyo ni kauli ya Waziri wa mambo ya Nje wa Kenya, Monica Juma ambaye wakati akihojiwa na Grace Kaneiya wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani baada ya taifa hilo la Afrika Mashariki kuzindua rasmi siku ya Alhamisi kampeni yake ya kuwania nafasi hiyo.

Waziri Juma ametaja miongoni mwa yale watakayoyazingatia ni uwakilishi wa kudumu wa bara Afrika kwenye Baraza la Usalama ambao kwa sasa haupo.

Halikadhalika Waziri Juma amesema kwamba katika ajenda yao wameweka mambo kumi ambayo watayapa kipaumbele iwapo watapata nafasi hiyo ikiwemo

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linaundwa na wajumbe 15 ambapo nchi 5 zina ujumbe wa kudumu na kura turufu huku 10 si wajumbe wa kudumu na hazina kura turufu na ujumbe wao huwa ni wa  kipindi cha miaka 2.

Nchi zenye ujumbe wa kudumu ni Marekani,  Uingereza, China, Ufaransa na Urusi.

Audio Credit
Assumpta Massoi/Grace Kaneiya
Audio Duration
5'16"
Photo Credit
UN Photo/Manuel Elías