Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao katika masomo ya Uanasheria - Hakimu Pamela Achieng

Wasichana ni majaji watarajiwa, wafuate ndoto zao katika masomo ya Uanasheria - Hakimu Pamela Achieng

Pakua

Maadhimisho ya kwanza ya Siku ya Majaji Wanawake duniani yalifanyika tarehe 10 Machi 2022, ikiangazia Haki katika Mtazamo wa Kijinsia.  Umoja wa Mataifa umeendelea kuadhimisha siku hii kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kuhakikisha usawa wa kijinsia na kushughulikia masuala ya uadilifu wa mahakama yanayohusiana na jinsia. Huku mkutano wa 68 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake duniani, CSW68 ukiendelea hapa jijini New York Marekani, nchini Kenya Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kupitia video iliyoandaliwa na washirika wetu Redio Domus amekutana na Pamela Achieng, Hakimu katika mahakama ya Ngong iliyo katika Kaunti ya Kajiado ambaye anaanza kwa kuelezea ni kwa nini kama mwanamke aliamua kuingia katika tasnia hii.

Audio Credit
Anold Kayanda/Selina Jerobon
Audio Duration
6'16"
Photo Credit
UN News