Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hata mimi mwenyewe nilikuwa sijiamini hadi nilipopata mafunzo ya RLabs - Mariam

Hata mimi mwenyewe nilikuwa sijiamini hadi nilipopata mafunzo ya RLabs - Mariam

Pakua

Mkakati wa Afya ya Uzazi kwa Wasichana, Haki, na Uwezeshaji nchini Tanzania (GRREAT) unaoungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wadau likiwemo shirika lisilo la kiserikali la RLabs Tanzania na serikali ya Canada ni mpango wa miaka mitano (2019-2024) ili kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuboresha ustawi wa wasichana balehe katika mikoa ya Mbeya na Songwe, pamoja na Zanzibar. Kupitia mpango huu wasichana wamepata zana na ujuzi wanaohitaji ili kuboresha maisha yao, familia na jamii zao. Mmoja wao ni Mariam wa Nyanda za juu kusini mwa Tanzania. 

Audio Credit
Assumpta Massoi/Mariam
Audio Duration
3'14"
Photo Credit
UNICEF TANZANIA